Jumuiya ya Sant'Egidio


Mwanzo Wake 
Sala
Uenezaji Injili
Jumuia Isiyokuwa na Mipaka wala kuta
Urafiki na Watu Maskini
Huduma kwa Ajili ya Amani
 
Text only
Home page
Select language

Jumuia Isiyokuwa na Mipaka wala kuta

Urafiki kati ya watu wa mataifa na mila tafauti ni njia ya kila siku ya kuendeleza undugu huu wa kimataifa katika Jumuiya ya Sant’Egidio. Ushirika huu wa kuishi pamoja kimataifa ina maana ya kuwa wazi kwa dunia nzima na pia kuishi katika familia moja, familia ya Mitume. 

Katika ulimwengu ambao mwisho wa milenia ya pili umezidisha vizingiti kati ya watu na kuchochea ubaguzi wa kitaifa na wa tofauti za mila na tamaduni, na ambayo ndiyo imekuwa chanzo cha migogoro mingi ya zamani na hata mipya. Jumuiya za Sant’Egidio zinashuhudia uwepo wa hatma sawa kwa watu wote, siyo tu kwa walio wakristu, bali kwa wanadamu wote.

Zipo Jumuiya changa sana na pia kunazo zile za zamani zaidi. Nyingine zina idadi kubwa sana ya watu na mizizi iliyopenya zaidi kuliko nyingine; nyingine nazo zinajulikana zaidi kwenye mitaa au sehemu zilipo, lakini zote kwa pamoja zinajitahidi kuwa, na kwa kweli ni familia iliyomzunguka Yesu.

Jumuiya ya Roma ndiyo Jumuiya kongwe zaidi ya zote. Ikiwa ni Jumuiya ya kwanza, inatoa huduma ya kuziweka pamoja zile Jumuiya changa bila kizingiti chochote "ila upendo" kama Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili alivyosema katika kumbukumbu ya miaka 25 ya Jumuiya ya Sant’Egidio mwaka 1993. Muungano huu unajieleza katika ushirika halisi na umoja kati ya ndugu, na ni muundo bora zaidi kwa maisha na shughuli za Jumuiya yenyewe.