Jumuiya ya Sant'Egidio


Mwanzo Wake 
Sala
Uenezaji Injili
Jumuia Isiyokuwa na Mipaka wala kuta
Urafiki na Watu Maskini
Huduma kwa Ajili ya Amani
 
Text only
Home page
Select language

Urafiki na Watu Maskini

"Kazi" ya tatu mahususi ya Jumuiya ya Sant’Egidio ambayo ni jukumu la kila siku tangu mwanzo ni utumishi kwa watu maskini, ambao pia ni wajibu wa kila siku tangu kuanzishwa kwake katika jukumu la kuishi urafiki. Vijana wanafunzi wa mwaka 1968 walioanza kukutana kwa ajili ya Neno la Mungu waligundua kwamba haingewezekana kamwe kuliishi mbali na watu maskini: watu maskini kama marafiki na Injili kama Habari Njema kwa watu maskini.
Kwa njia hii Jumuiya ilianza huduma zake kabla haijapata jina la Sant’Egidio. Wakati huo iliitwa "shule ya watu" kwa sababu haikuwa tu inatoa elimu ziada kwa watoto wahama-shule wa mitaa ya mabanda (kwa mfano mabanda ya "Cinodromo" kando kando ya Mto Tevere) mjini Roma, bali ilikuwa ndio chanzo cha urafiki kati ya watu tajiri na wale maskini. Tangu wakati huo, "shule za watu" zilianza kukua na kuongezeka Roma na katika miji yote ambamo Jumuiya inaishi, huku umuhimu mkubwa ukipewa hasa kwa wale wanaoishi katika hali zilizo ngumu zaidi. 

Kuambatana na sura ya 25 ya Injili ya Mathayo, urafiki huu uliweza kusambaa hadi kwa watu wa namna nyingine za umaskini: viwete, watu wenye akili pungufu, wasio na makao, wahamiaji maskini kutoka nchi zingine, wagonjwa, kambi za Wagypsi na za wakimbizi. Kwa miaka hii iliopita, kumekuweko kutafakari zaidi juu ya hali za umaskini ambazo hazikuwepo, hasa katika nchi za Ulaya ambako kwa mfano, wazee huishi hali ya upweke hata kama wanazo mali.

Jumuiya ya sant’Egidio hujiweka karibu na wale wanaochukuliwa kuwa duni zaidi, ikiwatambua kama ndugu pasipo ubaguzi wowote. Hao ni sehemu kamili ya Jumuiya. Kila palipo Jumuiya ya Sant’Egidio, kuanzia Roma hadi San Salvador, Cameruni hadi Ubelgiji, Ukraini hadi Indonesia, urafiki na kufahamiana na watu maskini zimekuwa daima shina lake. Hakuna Jumuiya, hata ile changa zaidi, ambayo ni ndogo au hafifu sana hata kutoweza kuwasaidia watu wengine maskini. Ni ile "hela ya mjane" iliyo na thamani kubwa zaidi mbele za Bwana (Mk. 12:41).