Huduma kwa Ajili ya Amani:
Kuifanya Dunia Kuwa na Ubinadamu Zaidi
Urafiki na maskini iliifanya Jumuiya ya Sant’Egidio kutambua vyema zaidi kwamba vita ndiyo hasa mama wa umaskini. Kwa njia hii upendo kwa watu maskini katika hali nyingi tofauti uligeuka kuwa kuwa kazi ya kutafuta amani, kuilinda pale inapohatarishwa, na kusaidia kuijenga upya kwa kuhimiza moyo wa majadiliano popote pale ambapo imevunjika. Njia ifanikishayo huduma ya kuleta amani ni kwa kutumia nguvu hafifu ya sala, kushirikiana hali ngumu za maisha, kukutana na kujadiliana.
APia, pale ambapo hali iliyopo hairuhusu kazi hii ya kuleta amani, Jumuiya hujitahidi kuleta ushirikiano kindugu kupitia misaada ya kibinadamu kwa raia wa kawaida ambao ndio wanaoadhirika zaidi katika vita.
Labda hizi ndizo sehemu ya shughuli za Sant’Egidio zinazofahamika zaidi, zinazozugumziwa sana kwenye vyombo vya habari. Lakini siyo mara nyingi utasikia vyombo hivyo vikitangaza shughuli zile za kindani za Jumuiya zinazotendeka daima za kufanya kazi pamoja na watu maskini, na kwamba Injili ndiyo mzizi wa kazi hizi.
Wanachama wa Jumuiya waliweza pia kuwa wawezeshaji na wapatanishi wa mazungumzo ya amani nchini Mozambiko na pia Guatemala, ambako vita vya kimauaji vilidumu kwa zaidi ya miaka 30.
Afrika na katika Balkan, na sehemu nyingine za Ulimwengu zilizojawa vita, zipo pia katika mawazo, nia na makusudio ya Jumuiya ya Sant’Egidio. Ilikuwa ni katika hali kama hizi ambapo imani ya Jumuiya ya Sant’Egidio katika "nguvu hafifu" ya sala na uwezo-kimapinduzi wa kuishi na kushawishi pasipo kutumia mabavu kutafuta amani ilipata kuzaliwa. Hizi ndizo fikra ambazo Yesu Kristu mwenyewe aliishi nazo hadi mwisho.

Kwa sababu hii, Jumuiya daima hushughulikia huduma ya kuleta uwelewano na mazungumzo kati ya madhehebu na imani mbali mbali. Tangu 1987 Sant’Egidio imejitolea kuanzia mashinani hadi kiwango cha kimataifa katika kupanga mikutano ya kila mwaka, kongamano na mikutano ya sala katika "Moyo wa Assisi".
Kwa kuitikia wito wa Assisi wa kulinda maisha katika hali zote, Jumuiya hii imejitolea katika kiwango cha kimataifa pamoja na mashirika mengine, kushughulikia shindikizo la kimataifa dhidi ya hukumu ya kifo katika mwaka wa 2000. Kampeni hii ni mnara mkubwa katika vita vya kulinda thamani ya uhai, na inawashirikisha wanachama wa Sant’Egidio kote ulimwenguni.
Mzizi huu huu wa Injili ndio shina la mipango mingine ya kibinadamu ambako wito huwaendea watu wote wenye nia njema bila kujali imani zao. Hii inahusisha pia Kampeni dhidi ya mabomu ya kutegwa ardhini, misaada kwa wakimbizi na kwa waadhiriwa wa vita na njaa kusini mwa Sudan, Burundi, Albania na Kosovo, juhidi za kuwasaidia watu wa Amerika ya Kati walioadhiriwa vibaya na tufani, na pia dhidi ya biashara ya utumwa kokote inapofanyika.
|
The School of Peace
in Kukes,
in the Kosovar refugee camp
|
|